Hospitali ya Pasiansi mbioni kukamilika

Na Kamati ya Mawasiliano,Kirumba

HOSPITALI ya Waadventista wa Sabato, Mwanza Adventist Medical Centre(MAMC),sasa iko katika hatua za mwisho za Ujenzi.

Kaimu Mkurugenzi wa Idaraya Afya ya Kanisa la Waadventista wa Sabato Jimbo Kuu la Kaskazini mwa Tanzania (NTUC), Dk Silas Kabhele, amesema zaidi ya shilingi bilioni moja na nusu zimetumika kujenga Hospitali hiyo.

Hospitali ya Pasiansi inavoonekana sasa
                                          
 Dk.Kabhele ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Afya katika Jimbo  la Kusinim wa Ziwa Nyanza(SNC) amesema Siku ya Sabato Mei 30 kwamba sasa zinahitajika takriban shilingi milioni 600 kukamilisha ujenzi.
Akizungumza wakati wa Huduma Kuu katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Kirumba Jijini Mwanza,Dk.Kabhele amesema Hospitali hiyo ya Gorofa tano tayari paa limeezekwa,kuta zote za nje zimepigwa lipu; na kwamba hata baadhi ya kuta za ndani zimepigwa lipu.
“Takriban shilingi bilioni 1.6 zimekusanywa kutoka kwetu na kutoka kwa rafiki zetu; kazi zilizobaki ni kumalizia lipu ndani, kuweka sakafu, madirisha, milango, kupakarangi, kuingiza umeme na maji na kusimika mitambo ya usalama”,Dk. Kabhele amebainisha.
Jengo la Hospitali ya Pasiansi limefikia hapa
 Aidha, amesisitiza kuwa Hospitali itakapoanza kazi, itakuwa kituo cha  Uinjilisti, ambayo ndiyo njia ya pekee ya kuisaidia jamii isiyomjua Mungu kuja wenyewe kwaYesu Kristo.
“Wale ,hujakutafuta huduma ya Afya; na hivyo hupata Injili itakayokuwa ikitolewa sambamba na huduma zetu za afya”,Dk. Kabhele amesisitiza. 

Akasema, "sasa Zinahitajika shilingi milioni 600 kukamilisha kazi hiyo ya Ujenzi wa Hospitali hiyo".
Jiwe la Msingi la Hospitali hiyo liliwekwa na Rais Jakaya Kikwete Septemba 8 mwaka 2013; na Hospitali hiyo ilitazamiwa kufunguliwa rasmi mwaka huu wakati wowote ikikamilika.
Akizungumzia vifaavya tiba,Mkurugenzi huyo wa Afyaamesema, tayari Kontena mbili za vifaa vimekwisha tumwa kutoka Uswisi, na Wajerumani wameahidi kuleta vingine kwa ajili ya kuanza kazi baada ya ujenzi kukamilika.
Kulingana na Kamati ya Ujenzi, kila Mtaa katika Jimbo la SNC umepangiwa goli lake.

 Hospitali hiyo itakapokamilika, itakuwa na vyuo mbalimbali vya Sayansi ya Tiba, na itakuwa na uwezo wa kuhudumia wastani wa wagonjwa 200 kila siku, pia itakuwa na jumla ya vitanda 450  vya kulaza wagonjwa.
Hospitali ya Pasiansi ikikamilika itafanana hivi
Aidha,Dk.Kabhele 
amewomba wadau wote wa Huduma za Jamii kuchangia mradi huu toka kona zote za nchi kuingiza michango yao katika akaunti ya ujenzi wa hospitali hii:
Jina la akaunti: Pasiansi SDA Hospital Fund,
Akauntinamba:      01J1060067500
Benki: CRDB


Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

4 comments:

 

Copyright ©2015 KIRUMBA ADVENTIST CHURCH