ZIARA YA PAPA MAREKANI NA AFRIKA.

“Mimi ni nani, hata niwahukumu mashoga?”
Conges Mramba na Mashirika ya Habari
KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani,Papa Francis amehitimisha ziara yake katika nchi tatu za Afrika zinazokabiliwa na hatari ya vita na Ugaidi,Kenya,Uganda na Jamhuri ya Afrika ya Kati(CAR),huku akiagiza haki za watu wote(wakiwemo mashoga)kulindwa na kuheshimiwa.
Akiwa Afrika ya Kati,Papa Francis amesema anatazamia kuona kila jamii inapewa haki bila kuachwa kundi lolote wakiwemo wapenzi wa jinsi moja-mashoga na wasagaji.
Msemaji wa Vatican,Father Federico Lombardi,amesema ingawa Papa hakutaja mashoga,lakini kauli yake ililenga hata wapenzi wa jinsi moja- homosexuals- haki zao kulindwa na kuheshimiwa.
Wakati wa ziara hii ya Papa Barani Afrika,wanaharakati wa haki za mashoga wamemwomba Papa kutangaza kwamba sheria kali dhidi ya mashoga katika nchi za Afrika ni haramu na hazifai kabisa.
Msemaji huyu wa Vatican amesema Papa hakukusudia kujihusisha chochote na mashoga katika ziara hii ya Afrika.
Jijini Kampala,Kiongozi huyu wa Kanisa Katoliki alikutana na vijana na wakimbizi, yatima na hata walemavu alipokuwa uwanja wa ndege.
Kwa muda mrefu sasa Papa amekuwa na msimamo unaoenda sambamba na kinachoitwa na Ulaya na Marekani, “Usawa na Haki kwa kila mtu,” wakiwemo wapenzi wa jinsi moja ambao hapa Barani Afrika wamekuwa wakikabiliwa na sheria kali.
Papa Francis alichaguliwa kuongoza Kanisa Katoliki Machi mwaka 2013.
Kwa miaka miwili sasa, amekuwa “MWAKILISHI WA MWANA WA MUNGU DUNIANI”(Vicar of Jesus, Vicar of the Son of God?)naam, Vicarius Filiidei! akijiungamanisha na masikini,wanyonge na sasa amekuwa akifanya ziara na kuwahurumia mashoga na kutaka sheria kali dhidi yao zilaaniwe.
Kufuatia hali hiyo,ziara ya Papa hapa Afrika imekuka wakati dunia ya Jumuiya ya Kikristo ikitakiwa kumtambua Papa kama Mwakilishi wa Yesu Kristo hapa Duniani,wakati baadhi ya watu wanapohoji mamlaka yake wakiuliza, “Papa ni nani?”
Alihitimu Chuo Kikuu cha Buenos Aires,Argentina shahada ya Kemia,kisha alisoma Falsafa Collegio Maximo de San Jose Centro Loyola,kabla ya kupata shahada ya Uzamivu(PhD)katika Theolojia huko Ujerumani.
Alikuwa kasisi Desemba 13 mwaka 1969; na akala kiapo cha upadrisho Aprili 22 mwaka 1973.
PAPA NI NANI HATA AHUKUMU MASHOGA?
Amekuwa wakiwakaribisha mashoga kanisani na watu wenye mitazamo chanya na ushoga huku akisema, “Mimi ni nani hata niwahukumu?”
Hii ndiyo kauli ya ‘Baba huyu Mtakatifu’ wa Kanisa Katoliki na msimamo wake dhidi ya ushoga,kwamba kuwatenga watu wa tabia hii makanisani na katika jamii ni sawa na kuwahukumu.
Naam, Mwakilishi wa Yesu(Vicar of Jesus) hapa duniani,anapojiuliza, “Mimi ni nani hata kuhukumu mashoga?” anaashiria zama za Kanisa la Kristo kuwabagua mashoga zimefika mwisho.
Siku chache zijazo,maaskofu,makasisi na wachungaji watakuwa mashoga bila kificho!
Naam Dhambi ya miji ya uwanda wa Sodoma na Gomorrah itahalalishwa duniani na makanisa.
Afrika Kusini,Ufaransa na mahali pengine,tayari kuna misikiti ya mashoga,kilichobaki ni baadhi ya mataifa ya Afrika kulegeza misimamo na kuhalalisha ushoga kama Ulaya na Marekani.
Kenya ni nchi ya kwanza hapa Barani kumkaribisha Papa huyu,mara alipowasili juzi uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta.
Papa huyu alimrithi Benedict XVI alipokuwa Kadinari wa Argentina akiitwa,Jorge Mario Bergoglio,amekuwa Papa wa 266 sasa baada ya Mtume Petro anayeitwa Papa wa Kwanza.
Kadinari Bergoglio alichagua jina la Francis I, kufuatisha Mtakatifu Francis wa Asisi mtu anayeshabiana naye sana kwa tabia ya unyenyekevu na kujishusha kwa watu wote.
Hivi anavyojishusha hata kwa mashoga na watu wa chini anasemwa kujidhili(simplicity); wanasma ni ‘kwa makusudi ambayo Kanisa linatakiwa kuondoa vizingiti vyote katika njia ya kumtangaza Bwana Yesu kwa Dunia’.
Papa huyu alizaliwa Desemba 17 mwaka 1936 kwa baba Mario Bergoglio na mama Regina Siyori aliyekuwa mama wa nyumbani. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa reli.
Waliishi Flores jirani na jiji la Buenos Aires.
Amekuwa akikwea nyadhifa kanisani tangu miaka ya 80 hadi Papa Paulo II alipomteua Askofu wa jiji hilo kuu la Argentina Mei 20 mwaka 1992.
Alikuwa kadinari Feburuari 21 mwaka 2001.
Sasa ni Askofu Mkuu wa Rome(PAPA)ambaye amezua mikanganyiko,akiongoza Wakatoliki bilioni 1.2 duniani kwa namna anavyoendesha mambo yake tofauti na watangulizi wake,walikataa kuwakubali mashoga kanisani na wale walioacha ndoa zao halali.
Mapapa waliomtangulia walisisitiza Wakristo kufuata ‘Njia Nyembamba’ inayobinya demokrasia,wakati huyu ni PAPA WA KUHESHIMU HAKI ZA MAKUNDI YOTE!
Hata amethubutu kuvunja itifaki za ulinzi ili awafikie watoto yatima,masikini na wanaodharauliwa na jamii.
Akiwa ziarani Marekani Septemba mwaka huu,alikutana na mashoga,masikini na wasio na makazi.
Kenya,amekutana na Waislam na viongozi wa madhehebu mengine ya dini akiwasisitiza kufanya maridhiano(kanisa Katoliki liliwahi kugombana na Waprotestanti sasa Papa anaomba kupatana nao na kusameheana),anasisitiza dunia iwe pamoja na mahali salama kwa kila mtu.
Amezunngumzia utunzaji wa mazingira akiwa Ofisi za UN mjini Nairobi,Gigiri.
Anasemekana kutowavumilia makasisi wanaowanajisi watoto.Kunajisi watoto wa kiume ni dhambi ambayo imekuwa ikiwatafuna makasisi wa kanisa hili,huku baadhi yao wakiomba waruhusiwe kuoa bila mafanikio.
Anatishia kuwachukulia hatua kali maofisa wa Kanisa hili watakaotumia ofisi zao kwa manufaa binafsi. Huyu ni Papa Mkali anayesemwa ndiye Kanisa Katoliki linayemtaka kutekeleza mipango yake.
Amekuwa hata akisafiri kwa usafiri wa umma.
Hata alipochaguliwa Papa alimuita mtu aliyemuuzia magazeti kila siku na kumwambia, “Asante,sasa nahamia mjini Rome”. Vatican city ni nchi ndani ya jiji la Rome.
Anasemwa kukataa uhafidhina ndiyo maana anawakaribisha mashoga,huku akisema hawezi kuwahukumu!
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani,Papa Francisco,alifika pia Washngton na kuzungumza na Kim Davis mmoja wa walio katika sakata la mashoga na wasagaji,kufuatia Mahakama Kuu kuhalalisha mambo hayo nchi nzima.
Makao Makuu ya Kanisa Katoliki,THE VATICAN,yalitangaza kwamba Papa alikwenda tu kukutana na mwanafunzi wake wa zamani,Yayo Grassi na familia yake,ambaye kwa hakika ni shoga wa Argentina(kwao Papa;walipotezana kitambo).
Msemaji wa Vatican,Kasisi Federico Lombardi,akasema Papa alikutana na dazeni ya watu katika Ubalozi wa Vatican mjini Washington,kabla ya kuondoka kwenda New York.
Akasema, kufanya mikutano na watu ni kitu cha kawaida tu kwa Papa huyu,sawa?
Na akaongeza kusema,Papa kukutana na Davis kwa muda mfupi mchana ule Ijumaa iliyopita, ilikuwa siyo dalili kuwa anakubaliana kwa vyovyote na ushoga ama usagaji wa akina Baba na Mama Davis.
“Papa alikusudia tu kuongea na mwanafunzi wake wa zamani na familia yake,basi”,Lombardi alifafanua.
Awali.hakufafanua huyu mwanafunzi alikuwa nani?
Kisha baadaye, picha ya video iliyowekwa kwenye mitandao ikaonesha Grassi akii ngia hapo Ubalozini,akiwa kamkumbatia mwalimu wake huyu wa zamani(PAPA FRANCIS),kisha akamtambulisha kwa ‘mshushu’wake huyu(shoga) ambaye tayari Papa alikwishamfahamu katika mkutano wa awali akiwa na marafiki wachache toka Bara Asia.
Ni hapa sasa, Msemaji Msaidizi wa Vatican,Padri Thomas Rosica,anapobainisha ni kweli huyu mwanafunzi wa zamani wa Papa huyu alikuwa Grassi,jamaa ambaye ni shoga.
Kwa hakika,Papa kama Kiongozi wa Kiroho,hawezi kukataa kukutana na watu mashuhuri kama viongozi wakuu(VIPs),Halafu akaja kuwabagua wengine kwa sababu ya dhambi zao,kama hawa mashoga.
Lakini,imebainishwa wazi,mkutano wa Papa hapa Ubalozini Washington ulikusudia kuwa wa hawa mashoga.
Kwa mfano, mmoja wa watu aliokutana nao,Davis ni Mkiristo wa Kanisa la Mitume(Apostolic Christian),aliyejikuta jela siku tano kwa kupinga mahakama kutoa leseni za mashoga,kufuatia Mahakama Kuu ya Marekani(Supreme Court)kuwa imehalalisha ndoa za mashoga nchi nzima hii.
Huyu alipinga kuhalalisha ushoga wa mumewe.
Baadaye Davis aliachwa huru baada ya Jaji kuonesha kuwa mambo yake hayakuleta madhara, alirejea kazini kwake.
Mwanamama huyu,Davis akiwa na mumewe walikutana na Papa hapa nyumba ya mwakilishi wa Papa Marekani(Nunciature)na akawashukuru hawa akina Davis kuwa majasiri!
Papa,aliwaunga mkono hao kwa sababu ya kile kinachoitwa, ‘Haki za Binadamu’ siku hizi ambazo kwa vyovyote ni pamoja na kuunga mkono haki za mashoga na wasagaji wa Marekani na dunia nzima siku hizi.
Mkutano na hawa akina Mama Davis na mumewe ulitakiwa ufanywe sirini na Papa,hata hivyo imesemwa kila mwanandoa alifanya mkutano na Papa kwa siri chumbani,chini ya Ulinzi Mkali wa ‘Vatican Security’,siri hii imekuja kubumburuka Papa alipokwishafika jijini Rome.
Kwa hiyo,Marekani watu wakashangaa Papa kukutana na hawa wanaoshadidia usagaji na ushoga,kuungwa mkono hivyo na Kiongozi huyo anayeheshimiwa mno duniani,kama Mrithi wa Mtume Petro.
Ilikuwa iwe siri,lakini vyombo vya habari vimefichua jambo hili la kukaa na kukubaliana na mashoga na wasagaji wa Marekani,nchi yenye mvuto wa kutisha wa uovu kama huu wa SODOMA na Gomorrah hapa duniani.
Balozi wa Papa mjini Washington,Askofu Mkuu,Carlo Maria Vigano,raia wa Italia maarufu kwa maskandali ya ‘VATILEAKS’ yaliyosababisha Papa Benedict XVI kuachia ngazi.
Huyu Askofu Mkuu alitoa siri ya ufisadi wa mamilioni ya Yuro hapo Makao Makuu ya Dini Kuu duniani,baadaye alihamishiwa Washington,baada ya Benedict kuachia ngazi.
Davis alikuwa na kampeni mahususi,na huyu Vigano akiwa anahutubu Chuo Kikuu cha Notre Dame mwaka 2012,akisema Mtaala wa shule ulikuwa ukiunga mkono ushoga na usagaji ambao ni kawaida na wenye afya!
Sasa kanisa linajitetea kwamba,PAPA awaliwajua watu aliokutana nao Ubalozini kwa majina tu,wala hakujua sana mambo yao ya ndani.
Watetezi wa kitendo hicho cha Papa na mashoga na wasagaji wanasema,ilikuwa bahati mbaya hivi;kwani Papa hakujua alikutana na watu wa namna gani?
Na sasa kitendo hicho matokeo yake yamekuwa hasi hapa duniani,kwamba Papa ameanza kucheka-cheka na mashoga na wasagaji,kwa madai ya kuheshimu,HAKI ZA BINADAMU.
“Kama mtu hawezi kuwapa ruhusa wengine kupinga jambo kwa uangalifu,basi anapinga Haki”,Papa anasema.
Ni kama anakubali kuwaruhusu watu ‘Kupinga Amri 10 za Mungu’ zinazopinga ushoga na usagaji,kwa uangalifu.Anasema kufanya hivyo ni kupinga haki.
Kusema hivyo maana yake ni kwamba,PAPA Francis sasa anakuwa mwangalifu kuwapinga watu wanaokubali ushoga na usagaji.
Ndiyo maana anakutana nao kwa siri na kujadili masahibu yanayowakuta hata kama ni wanandoa kama huyu mama Davis.
Huyu Papa Francis,jina hili kwa Kilatini ni Franciscus, Kiitaliano ni Francisco.
Alipozaliwa huko Buenos Aires,Argentina Desemba 17 mwaka 1936 walimwita,Jorge Mario Bergoglio,sasa ndiye Papa wa 266 wa Kanisa Katoliki.
Ndiye Askofu Mkuu wa Rumi(Rome)na Mkuu wa nchi, Vatican City.
Ni mmoja wa Jesuits(society of Jesus)chama alichoanzisha Ignatius Loyola.(SOMA Great Controversy)
Alikwenda kusoma seminari,akapanda vyeo hadi kuwa Askofu Mkuu wa Buenos Aires mwaka 1998,alikuwa kadinari 2001 wakati wa Papa Yohana Paulo II.
Huyu ndiye aliyemrithi Papa Benedict XVI wakati anajiuzulu Feburuari 28 mwaka 2013,alipochaguliwa na ‘Conclave,’ baada ya Moshi Mweupe kuwaka viwanja vya St .Peters.
Jina lake la Kipapa, ni kwa heshima ya Mtakatifu Francis wa Assisi.
Huyu ni papa wa kwanza kutoka Amerika,na wa kwanza papa asiye wa Ulaya tangu Gregory III Toka Syria,mwaka 741 AD.
Hapa wanaofuatiliamsimamo wa kanisa hili kuhusu uvunjaji wa ndoa(talaka)na mfungamano miongoni mwa mashoga na wasagaji sasa unapewa msimamo mwepesi.
Kanisa hili lilitegemewa kupinga uvunjaji wa ndoa na dhambi hizi za Sodoma,sasa kuna kila dalili Jamii ya Kikristo kote Ulaya na Marekani,kuruhusu uchafu huo kuingia kanisani,kwamba ndiyo Haki stahiki za Binadamu!
Kanisa linakwenda kushirikiana na wakuu wa dunia kuridhia dhambi za miji ya uwanda,ili kutengeneza Uhuru wa watu dhidi ya Mungu wa mbinguni?
Huku wakiuliza maswali, ‘Binadamu ni nani hata awahukumu wengine?’
USHOGA IRELAND
Hakuna lugha nyingine ya kusema jambo hili,ila kueleza kwamba Ireland, nchi ya WAKATOLIKI ambao ni asilimia 87 wamekesha Jumamosi moja Mei mwaka 2015,kushangilia Ndoa za Mashoga na wasagaji kukubaliwa nchini humo.
IRELAND kuna watu 4,593,100 na kati ya hawa,takriban asilimia 90 ni Wakristo wa Madhehebu ya Katoliki,wakati madhehebu mengine kama Church of Ireland ni asilimia tatu,na mengineyo ni asilimia tatu pia.
Sasa,Jumamosi ,Mei 23 mwaka huu 2015,katika mji Mkuu wa Dublin watu walikesha usiku mzima wakifurahia kura ya maoni, “Referendum” kuwapa ushindi mkubwa mashoga na wasagaji kuoana.
“YES CAMPAIGN” waliibuka na ushindi mkubwa,kuashiria sasa nchi hii imefanya ‘MAPINDUZI’ makubwa ya Kijamii(SOCIAL REVOLUTION)dhidi ya Bwana mkubwa Yehova,anayepinga (kupitia AMRI 10),Mashoga na wasagaji kuoana.
Wanaounga mkono Ndoa za Jinsi moja, “Yes campaign” wamepata asilimia 62 ya kura zote zilizopigwa,wakati “No Campaign” waliambulia asilimia 38 tu ya kura.
Huu ni ushindi wa kishindo wa Ibilisi dhidi ya Bwana Mungu,kuhusu suala hilo la hatari hapa Duniani..
Katika Mambo ya Walawi 18:22 BWANA aliwaambia watu wake,
“Usilale na Mwanaume mwenzako kama ulalavyo na mwanamke(ngono),ni machukizo(kwa Mungu); na usilale na mnyama(fungu la 23).
Hii ndiyo DHAMBI YA MIJI YA UWANDA wa Sodoma na Gomorrah,iliyosababisha Mungua kuangamiza miji ile jirani na Bahari Mfu(Dead Sea).
Naam,Ireland inafuata nyayo tu za mataifa mengi hapa Duniani kuhalalisha wanaume na wanaume,au wanawake kwa wanawake kuoana.
Amri za Mungu ambazo zimekuwa zikikumbatiwa na mataifa ya Bara la Afrika, zinasema ‘Ndoa’ ni muungano wa hiari kati ya mtu mme na mtu mke,basi.
Hata hivyo,Afrika Kusini,kupitia Katiba ya Nchi hii,inaruhusu mashoga kuoana(Hommosexuality),na wanawake kuwaoa wanawake wenzao(lesbianism).
Kana kwamba hili halitoshi,Rais wa Marekani,Barack Obama na Waziri Mkuu wa Uingereza,David Cameron,akaamuru nchi za Afrika kubadili Katiba zao na kuruhusu ‘MAPINDUZI’ haya- social revolution-dhidi ya AMRI ZA MUNGU!
Marekani,ushoga na usagaji sasa ni kitu cha kawaida sana;wanaume na wanawake wanakiri kuwa na uhusiano wa kimahaba na wenzao wa jinsi moja-same sex,hata kama si kufunga ndoa.
Wengine wamefanyiwa Operesheni kubadili jinsi ili waoe au kuolewa-Mungu nadhani kachokwa katika nchi hizi zinazojidai za demokrasia.
Kichwa kimoja cha habari kikasema:
“IRELAND MIGHT JUST HAVE BECOME A GREAT LITTLE COUNTRY IN WHICH TO BE GAY!”
Ushoga sasa ni mtindo wa leo wa kuifanya nchi inayoridhia kuwa ‘Kubwa’.
Angalia,matokeo ya kura za maoni, ‘referendum’, yaliyotolewa kwa waandishi wa habari mjini Dublin Jumamosi hiyo,yalisema kwamba kura 1,201,607 zilipenda ushoga,na ni kura 734,300 tu zilizopinga,Riona Ni Fhlanghaile ofisa wa Uchaguzi alisema.
Tumesema awali kwamba Ireland ina watu takriban milioni 4.6.
Kwa kawaida, nusu ya watu hujiandikisha kupiga kura katika nchi yoyote,na nusu ya ile nusu ndiyo wanaopiga kura,sasa waliopiga kura ni milioni mbili,na zaidi ya nusu wamekubali USHOGA!
Hii ni sawa na kusema zaidi ya asilimia 60 ya wananchi ambao wengi ni Wakatoliki,wameunga mkono ushoga na usagaji! Hii ni kwa mujibu wa Afisa wa Uchaguzi, Fhlanghaile.
Kampeni ya kuunga mkono Ushoga, “YES CAMPAIGN” ilikuwa kali mno, hata watu waliotaka kuipinga,waliona aibu wakajikuta wanapiga kura ya ‘NDIYO’kwa ushoga.Hii ni kwa mujibu wa Gazeti la The Guardian la Jumapili, Mei 24 mwaka huu.
Nataka nikwambie msomaji,Ireland ina watu wengi WAKRISTO(wawe Katoliki ama wengine)ambao sasa wanaona Ushoga siyo Dhambi,ni uhuru tu na usagaji ni poa tu!
Hata maaskofu ni mashoga.
Kwa hiyo, sheria za Mungu zilizowatesa watu siku nyingi kuwanyima uhuru,zimeshindwa,watu wakashangilia usiku mzima mjini Dublin.
Wanashangilia,Mungu kushindwa na sheria zake kandamizi,zinazowanyima watu UHURU na DEMOKRASIA,siyo?
Jambo kama hili la uasi dhidi ya Maagizo ya Mungu(Agano Jipya na Agano la Kale)liliwahi kutokea katika karne ya 10 huko mjini Paris.
Watu walishangilia sana Biblia ilipokataliwa,na watu wakasema Mungu hayupo.
Ni katika kile kiitwacho -FRENCH REVOLUTION.
Ukitazama Ufunuo wa Yohana 11:8-10 kuna kitu kinachoshabihiana na kilichotokea Dublin,Mei 2015.
Mashahidi wa Yehova,Agano la Kale na Agano Jipya, ‘wameuawa’ katika mji mkubwa uitwao kwa mafumbo, SODOMA na MISRI,maiti zao hazikuzikwa kwa siku tatu na nusu za mafumbo,watu wakafanya dhihaka dhidi ya maiti hizo(maagizo ya Mungu),lakini watu wa mji ‘WAKASHANGILIA’ sana,wakafanya shangilizi,na kupeana zawadi!
Sodoma na Misri(zama za Farao)walimkataa Mungu kwa namna hii hii.
Sababu?
Ngoja. Ufunuo 11:10 husema, “Mashahidi wa Mungu”,yaani neno lake,Biblia,Agano Jipya na la Kale, “liliwatesa” watu wote wakaao juu ya uso wa dunia.
Biblia,inawatesa watu kuwakataza uzinzi,kuwakataza rushwa,uchafu,uongo,mauaji n.k
Biblia inayowanyima watu uhuru,inayosisitiza kuwapo kwa Mungu na sheria zake za kuingilia uhuru wa watu,inapokataliwa,watu hushangilia sana kama hao wa Dublin, ambao sasa wanaishi kwa uhuru,bila kitisho cha Mungu kuchoma mji wao unaoitwa ‘Sodoma ya Siri!’
Haya niyaache kwanza.
Nataka kusema kwamba,Asilimia 62 ya wa Irish,wamechagua ushoga kuendelea bila kitisho katika nchi yao.Mtu mume akipata mwanaume mwenzake wakakubaliana.
“John sasa wewe ‘Wife’wangu,mimi ndiye Mume wako, hakuna ‘Michepuko’ sawa?”
“Poa tu!”
Haya, Mwajuma naye akimpata Jasinta,wanasagana,wanaoana basi! Uhuru,Demokrasia,Haki za Binadamu,Haki za Kiraia,Mapinduzi ya Kiraia-social revolution n.k
Matokeo ya kura hiyo yanaonesha wakatoliki wamekataa maagizo ya Maaskofu na Kadinali waliyokariri katika Biblia kuwa ushoga na usagaji ni marufuku!
Gazeti la The Guardian na Shirika la Habari la CNN limesema kura nyingi za ‘NDIYO’ kwa ushoga,maana yake ni safari ya Ireland kuelekea kinachoitwa,JAMII HURU, Liberal and secular society.
“ to Liberalize” ni kuweka HURU(to set free) kutoka ‘dhana’ ya kuwepo Mungu duniani, kwa sababu ‘secular’ ni kuondoa dini, ‘not religious or spiritual’ kwa hiyo WAKATOLIKI nchini Ireland wamekataa kufuata DINI ama mambo ya kiroho yanayomhusu Mungu.
Uamuzi wa kumpinga Mungu mjini Dublin umepokelewa kwa sherehe kubwa mitaani,(the massive street party)na mashoga wa mji huu.
Jumapili,nikitazama Aljazeera na BBC World asubuhi,nikiandaa makala hii, nikaona kwamba Enda Kenny akisema matokeo ya kura za kuruhusu ushoga humaanisha watu wengi katika Jamhuri hii wamejisimamia,kwa siri katika masanduku ya kura,wametoa tamko, ‘public statement!’
Jamii ya Dublin imeamua kuwaona mashoga na wasagaji kuwa ni binadamu sawa tu,na wanalazimika kupendwa.
Naibu Waziri Mkuu wa Ireland na Kiongozi wa Labour,Joan Burton akasema watu wa Ireland wamepiga teke kali unyanyapaa na ubaguzi(wa Biblia)dhidi ya Mashoga.
Alimnukuu HARVEY MILK,Mwanasiasa na mtetezi wa Haki za Mashoga(LGBT rights) aliyesema, “Matumaini hayatakuwa kimya”.Sasa yamesema huko Ireland,yalishasema Ulaya na Marekani karibu nzima,yanathubutu kusema Afrika,Wafrika wanaonekana wagumu,kizazi kilichozaliwa miaka ya 1960 na 70 kikiisha,ushoga unakubaliwa AFRIKA.
WATU WA VIJIJINI ndiyo bado ngome(stronghold) ya Mungu inayopinga ushoga na usagaji,lakini watu wa mjini,hawa wanakubali mabadiliko mtu kuvunja ndoa anavyotaka na utoaji mimba viruhusiwe tu.
Dini ya mjini na ile ya vijijini,vimeanza kugombana.Mjini Wachungaji sasa wamesoma sana,wametoka Ulaya na Marekani, na mambo haya MACHAFU SANA,wameyajaza Makanisani na misikitini,sasa wanasema vijijini hawakusoma sana hawajui dini vizuri,walikaririshwa dini ya kizamani!
Waziri wa Afya,Leo Varadkar,shoga wa kwanza waziri ndiye aliyesoma matokeo ya kura hiyo ni MAPINDUZI YA JAMII(Dhidi ya Mungu).
.Sasa wanataka iwe hivi:
“Marriage may be contracted in accordance with law by two persons without distinction as to their sex.”
Mtu akijisikia kuoana na mtu wa Jinsi sawa na yake,wewe Padri,Sheikh au Mchungaji unamkataliaje?
Mbona Mapadri wengine na maskofu ni mashoga?
Ndiyo maana Ulaya na Marekani sasa kuna misikiti na makanisa ya mashoga.
Bendera ya Upinde wa Mvua ya Mashoga ilianza kuinuliwa karne ya 18,wakati sheria ya ndoa inayomtambua mume na mke tu ilipoaza kupingwa. Kuna picha nyingi za mashoga na wasagaji wa Ireland wakibusiana hadharani kuanzia Jumamosi usiku.
“The battle is not over. There are countries throughout Africa and Asia in which it is terribly dangerous to be gay,”
Norris ameisema Afrika na Asia kuwatisha wapingamashoga,kwamba sasa vita imeanza,Ole wenu Afrika,ambako mtu kuwa shoga eti ni issue...
“It’s wonderful. It’s a little bit late for me … I’ve spent so much time pushing the boat out that I forgot to jump on, and now it’s out beyond the harbour on the high seas. But it’s very nice to look at.”
Hii ni kauli ya mashoga wakiona bado kitambo Dunia nzma itaimba kishoga,itatembea kishoga,ngoja tu.
Kwa ushindi huu,mashoga wamesema Vatican imepigwa mweleka mkali,bado wengine,Waislam au maprotestanti.
Vijana sasa wameamua kuondoa dini na Mungu mwenye dini katika akili zao.
Kukubali ushoga eti ni LOVE AND EQUALITY.
Wengi lazima kukubali mambo haya.
Kwa kifupi,ushindi huu ni ‘BIG MESSAGE’ dhidi ya wanaopinga ushoga,ni ‘sweet victory’ dhidi ya Mungu na watu wake.
Biblia na Vitabu vingine vitakatifu vinavyopinga ushoga,vimepigwa kumbo kwa ushindi wa kishindo,bila shaka Mungu anashika tama,na watu wampendao wanashangaa kuona shangilizi za Dublin juzi zimefika hadi Dar es salaam,Mwanza na Arusha.
VITA BADO MBICHI, wakristo,waislam changamkeni mkainue vichwa vyenu juu.

Kwanini waovu wanapendwa na kulindwa sana na Mungu kuliko Wema?


Kwanini waovu wanapendwa na kulindwa sana na Mungu kuliko Wema?
• Vyombo vya ghadhabu vinaruhusiwa kutekeleza agenda zake!
Na Mwandishi Maalum,Kirumba
MKURUGENZI wa Vijana,Muziki na Chaplensia katika Union ya Kaskazini mwa Tanzania(NTUC),Pr.Elias Kasika, amewataka wa-Adventista wa Sabato kushukuru na kustahimili mema na mabaya yanayowatokea,kwa kuwa Mungu anaruhusu kila jambo litokee kwa makusudi ya wokovu.
Akizungumza katika Ibada maalum ya shukrani kwa Mungu katika kanisa la wa-Adventista wa Sabato Kirumba Jijini hapa, Novemba 28 amesema kwamba haiwapasi wanadamu kumlaumu Mungu kwa kuwa waovu wakiwemo mafisadi wanalindwa na Mungu kuliko watu wenye haki.
“Wabaya wanalindwa na Mungu hata watakapomaliza kufanya kazi yao ya ubaya,maana waongo na wadanganyifu kama Yakobo walipendwa sana na Mungu kuliko hata waaminifu kama Esau”,alisisitiza Pr.Kasika huku akikariri Biblia takatifu katika kitabu cha Mwanzo,Warumi na. Zaburi.
Akawashauri wenzi wa ndoa kumshukuru Mungu hata ndoa zao zinapoingia katika machafuko,ili agenda ya Mungu ipate kutekelezwa.
Hapa,Pr.Kasika alikuwa akikemea tabia ya watu kutengana ama kuachana na wenzi wao wa ndoa kwa kisingizio cha ukatili,ubaya na hiana miongoni mwao.
Akasema pia kwamba hata wanasiasa wanakasirika na kuiingiza nchi yetu katika vurugu kwa kushindwa kutambua kwamba Mungu ndiye atawalaye katika dunia,na agenda zake zinapaswa kutekelezwa wakati wa Pambano kuu baina ya ubaya na wema.
“Kaini alikuwa chombo cha ghadhabu,alipewa fursa kutenda mema akachagua kumuua nduguye Abeli aliyekuwa mwema,lakini bado Mungu alimwekea ulinzi ili asiuawe.Watoto wa Kaini Mungu aliwalinda na kuwapa ujuzi na vipawa vya muziki wa hali ya juu na uwezo wa uhunzi”,Pr.Kasika alisisitiza.
Amehoji kama wataalam wa teknolojia ya hali ya juu wote ni waaminifu,lakini akasema Mungu huwabariki hata waovu wanaofanya maajabu katika dunia leo, hata hivyo waaminifu wa Mungu wanapaswa kushukuru kila jambo.
“Kama watu waaminifu hawataki kushukuru kila jambo,basi huenda wanaweza kuliacha kanisa wa wakaamua kuasi”,amesema,huku akieleza mateso aliyopata Paulo wakati alikuwa mtumishi mwaminifu wa Mungu.
Amesema pia kwamba,wala si ajabu kwa watu waaminifu wa Mungu kupata ajari,kufa au kuvunjika miguu wakiwa katika kazi ya Mungu,kwa kuwa vyombo vya ghadhabu(uovu)vimeruhusiwa kuendelea kufanya kazi duniani.
Akahoji, ‘Ni wangapi watakaomshukuru Mungu katika mabaya yaliyotokea? Je,kama wewe ni mume au mke,utakwendaje kumshukuru Mungu kwa sadaka za shukrani kama hujamsamehe kwa mabaya aliyokutendea?”
“Pendo la Mungu linakuongoza kwa kukuumiza ili ufikirie kuungama,siyo kulaumu na kushindwa kumsamehe mwenzako aliyekuumiza!” Pr. Kasika alisisitiza.
Baadhi ya wageni waliohudhuria katika ibada ya jana Kirumba ni pamoja na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza,Miraj Mtaturu, Mbunge wa Ilemela(CCM)Angelina Mabula,Mwenyekiti wa Jimbo la SNC la wa-Adventista wa Sabato,Pr.Zadock Butoke,Mkurugenzi wa Afya wa NTUC,Dk.Silas Kabhele,Mkrugenzi wa Mawasilano wa SNC,Pr.Beatus Mlozi ,viongozi wastaafu wa serikali na madiwani mbalimbali katika jiji la Mwanza.
Akitoa shukrani,Katibu wa CCM mkoani Mwanza,Miraj Mtaturu amesema Kanisa la wa-Adventista wa Sabato ni sehemu ya Jamii ya wa-Tanzania wanaopaswa kuthamini umoja.
Amesema kuwa kiongozi wa umma ni kuwa mtumishi wa Mungu katika sekta za umma,akaomba kanisa kuwaombea kwa Mungu,kwa kuwa unapogusa maslahi ya watu wabaya ambao ni wachache kulinganisha na wengi wabaya.
‪#‎SHARE‬ NA WATAKATIFU WENGINE WA BWANA

Wasabato waishio Ughaibuni kusali Kirumba Desemba 26

Na Kamati ya Mawasiliano

Washiriki wa Kanisa la wa-Adventista wa Sabato waishio Ughaibuni,watakuwa na program maalum Desemba 26 mwaka huu katika Kanisa la wa-Adventista wa Sabato Kirumba Jijini Mwanza
Uongozi wa Kanisa la Kirumba,umethibitisha wageni hao kutoka ng’ambo na nje ya jiji la Mwanza kusali Kirumba na kuendesha program maalum kanisani hapo tangu asubuhi hadi jioni.
Uongozi wa kanisa hilo umewataka washiriki kuwasiliana na uongozi wa kanisa hilo kama kutakuwa na ndugu,rafiki ama mtu yeyyote aliyeko ng’ambo atakayetaka kushiriki program hii adhimu kanisani hapo.

Marekani yaidharau Biblia

    Na Conges Mramba
BAADHI ya wagombea Urais wa Marekani kupitia chama pinzani cha Republican,wamesema kitabu kitakatifu,Biblia ni ‘filamu tu ya kufikirika’ iliyojipatia umaarufu;na aslani haina ukweli wowote!
Donald Trump, anayewania kuteuliwa na chama hicho kuwa Mgombea Urais mwakani,amemkosoa Mgombea mwenzake kupitia chama hicho,ambaye ni muumini wa Madhehebu ya  wa-Adventista wa Sabato,Ben Carson, kwamba Biblia anayotumia kufanya kampeni si chochote si lolote bali,ni filamu iliyopata sifa tu, “Great Movie”.
Alikuwa akizungumza  katika mahojiano na David Brody wa Shirika la Utangazaji la Christian Broadcasting Network, Septemba mwaka huu,akasema Agano la Kale na Jipya(Biblia yenye vitabu 66) ilitokana na Kilatini na Kigiriki cha zamani, “Biblia” maana yake, “Vitabu” ama Kitabu.
Trump,alikuwa kama anajibu mapigo baada ya Ben Carson kujitetea kuhusu kukosa uzoefu wa kisiasa, akajifananisha na Nuhu alivyokuwa hana uzoefu wa kazi ya uselemara,lakini akaja kujenga safina iliyokiokoa kizazi chake katika gharika(Tazama kitabu cha Mwanzo sura 6-9).
Taaluma hiyo ya Ujenzi wa Safina hufananishwa na ile Wazungu waliyotumia kujenga meli kubwa ya Fahari iliyozama mwaka 1912 huko Uingereza, Titanic. Meli kubwa ya Titanic ilizama huko Bahari ya Atlantic.
Tuijadili kidogo Titanic.
Titanic, iliitwa “The Unsinkable” kwa sababu ilithibitishwa kutozama kwa namna yoyote.
Basi,ilizama kwa sababu ya Ibilisi na maajenti wake Freemasons.
Saa nne na dakika 20.
Ni usiku wa manane wa Aprili 15, mwaka 1912. 
Hukuwepo na mimi sikuwepo, wakati huo-imepita miaka 103 kamili.
Titanic ilianza kupotelea katika mawimbi makali ya Atlantic.
Ilikuwa meli ya fahari sana kupita zote wakati huo,iligonga Mlima wa Barafu,ikaanza kupoteza mwelekeo wake.
Jumla ya watu 1,503 hatimaye walikufa katika ajali ile ya kihistoria, na kulikuwa na majeruhi wengi.
Ajali mbaya zaidi ya meli duniani ni ya Feburuari 26,mwaka 1916 meli ya Provence ya Kifaransa ilizama Mediterranean na kuuaa 3,100.
Kwanini haikumbukwi? Hii nayo ‘cha mtoto’.Uchina waliwahi kufa watu 6,000 katika ajali ya meli mwaka 1948,lakini watu hawaambiwi haya,isipokuwa Titanic tu.
Meli hii Titanic Unsikable,ilikuwa na uzito wa tani 46,500, ilianza kuzama polepole katika muda usiopungua saa tatu hivi.
Iliundwa imara sana,lakini ‘Unsinkable’ ilizama na kukomesha kiburi cha watu cha utajiri.
Ilikuwa na kimo cha futi 883.
  Jioni, Aprili 14 mwaka huo 1912 meli hiyo ikiwa safarini baharini Atlantic ilikuwa ikipasua mawimbi shwari kabisa.
Ilikuwa ikienda jijini New York, Marekani na ilitokea Southampton,Uingereza. 
 
Meli hii iliambiwa kwamba baharini kulikuwa na mabonge ya barafu, hawakusikia.

Ni hapa tunapoambiwa,Nahodha wa meli alipewa maelekezo kuwazamisha watu fulani waliokuwemo melini,kwa sababu ambazo wao Freemasons walizijua.
Kama maili 20 hivi nyuma ya Titanic kulikuwa na meli nyingine ikija-CALIFORIAN- ikazima injini zake,ikichelea kugonga milima ya barafu na kuvunjika kisha kuzama.
Titanic waliziba masikio.
Ni kawaida kwa Aprili na Mei baharini kuwa na milima ama mabonge ya barafu makubwa na marefu mno.
Mchana saa 5:40 tayari Titanic ilikwishapinduka na ijini zake zilikwishaipeleka harijojo.
Kulikuwa na meli nyingine(The White Star Line) ya kuratibu safari za Titanic ilikuwa ikikatisha bahari ya Atlantic,haikufua dafu ili kuzuia Titanic isizame,maana ilikuwa kwa maelekezo ya Freemasons.
Angalia, abiria waliambiwa meli ilikuwa inazama,wakakataa kuingia katika boti za uokozi.Waliendelea kucheza muziki mtamu na kukamata ‘Kilaji’ tu, wengine walifunga ndoa humo-walipuuza onyo. 

Wanafananishwa na wale wa zama za Nuhu na wale wanaodharau kuwepo Mungu.
Niliwahi kuona Filamu moja kwamba kulikuwa na maharusi mle,mmoja akafa mwingine akanusurika, Titanic ilikuwa na starehe zote ndani, ndiyo maana watu walioambiwa wajiokoe wakakataa. Hawakuamini “Unsinkable” ingezama hata siku moja.
Wanaume walikataa kupanda boti za uokozi wakasema wanawake na watoto kama waliogopa basi wapande hizo boti, “Haitazama!’ walisisitiza.
Walisalia ndani ya meli hii hadi ilipozama kabisa vilindini,mashua zikajaa watu wengi,wao wakakosa nafasi hatimaye.
Meli ya Uingereza, Carpathia,ilisikia mlio wa kuomba msaada ikarudi na kupita eneo lile la ajali.Iliokoa watu 712 tu waliokuwa katika zile mashua za TITANIC ILIYOKWISHAZAMA.
Eneo la ajali hii ni karibu na Pwani ya New Foundland. Hii Titanic-white star-nyota nyeupe ilikuwa ya Uingereza,na ilizama kwa maelekezo ya Freemasons,kulikuwa na MATAJIRI ambao ilikuwa hapana budi wafe kama Freemasons walivyotaka,nahodha alipewa agizo.

 Sijui unaelewa?
Meli hii inaacha simulizi, naomba mtafute habari zake, msinisumbue kwa maswali.Titanic inafananishwa na kuzama kwa dunia hii,watu wanaambiwa ajali inakuja,hawasikii ya wahubiri.
Tazama Luka 21:35 utaona zama za Gharika ya Nuhu. Duniani kuna vita siku hizi Luka 21:9,10 na ni vita kuu ya dunia inayoongelewa hapa hadi Luka 21:11
Simulizi hii ya Biblia  leo hufananishwa na Titanic iliyozama mwaka 1912 kama tulivyoona.

CARSON CHIZI?
Ben Carson, mtaalamu bingwa wa upasuaji wa mishipa ya fahamu na magonjwa ya akili,amekuwa akidhihakiwa kwa kauli yake ya kutumia mifano ya Biblia,kitabu kinachofananishwa na hadithi za  kale za uongo za kujitungia(Myth),ambazo hazibebi uhalisia wa maisha ya mwanadamu siku hizi.
Trump ambaye anaona Biblia kama kisasiri(novel)alisema kitendo cha Benjamin Carson kujifananisha na Nuhu wa Biblia siyo kichekesho,bali anataka kusema kwamba,kama Mungu alivyomtuma Nuhu kuanzisha maangamizi kwa binadamu(gharika),basi sasa amemtuma Ben Carson kuwa Rais Marekani!
Wamerekani wanaamini sana teknolojia na falsafa za watu kama Charles Robert Darwin,mwasisi wa dhana ya uibukaji, “Big Bag Evolution’ na mawazo ya Mungu kutokuwepo,au kama yupo eti hana mamlaka na utawala wa dunia.
Akasema,ni kama kutumia hadithi za kufikirika za Biblia na akili za watu wanaoshika imani kupita kiasi kama huyo Carson aliyewahi kuandika kwamba Uibukaji(evolution)ulihamasishwa na Shetani.
Wagombea Urais wa Republican sasa wanatumia ‘hadithi za kufikirika’ ndani ya Biblia kama kitabu kilichofanikiwa kukaa millennia nyingi tangu nchi za Mashariki,Ulaya na Marekani na kughubika akili za watu wakazishika.
Katika mitandao ya kijamii,David Sirota,akasema Wamarekani sasa wanaishi katika unafiki wa kutisha wa dunia wanaozungumza katika lugha ya kutia mashaka,badala ya kusema watu wanachofikiri.

“Watu wote wanafanya kinyume cha wanachohubiri makanisani na misikitini,tunajidanganya nafsi zetu katika kusaka fedha..”alisema mchangiaji huyo wa kauli ya kuibeza Biblia.

Akasema hata serikali ya Marekani inatafuta pesa,Mabenki ya Wall Street, matajiri wenye pesa Marekani wanasaka pesa tu
Hata maadili mema ya Biblia yalishasahaulika,Amri 10 za Mungu zimetupwa,ni maneno katika makaratasi yanayoitwa,Biblia.
Akasema, “Kama tungekuwa waaminifu kwa Biblia,tungekwishaacha vita visivyo na faida(duniani),tungeacha kutafuta pesa,badala yake tungeitunza nchi yetu(Marekani/,watu wake na  kudhibiti deni letu kubwa kwa nchi za nje”,alisema mchangiaji huyu katika twitter.
Akasema yeye aonavyo,Biblia ni kama kitabu tu cha kukuongoza namna ya kuishi ,na kamwe siyo kitabu kilichoandikwa na mkono wa Mungu,watu watakwambia maneno mengi ya Biblia wakati hawajui hata maana yake!
Akasema watu wawe makini na Biblia,na wasiwaamini wachungaji.
Amesema anaamini kuwepo Mungu,lakini kila mtu anahaki ya kuchagua kuwa mwema au mwovu,lakini mwisho wote watarudi kwa Mungu huyo huyo,akawaambia Marekani kuwa macho na akina Ben Carson washika dini kupita kiasi waliokosa akili,wanaonga’ng’ania hadithi za Biblia.
Wanasema Mungu aliyedharau watu baada ya kuwaumba,akamtuma mtu wa miaka 600,Nuhu kutengeneza Safina kwa karne moja,akaleta gharika ya maji kwa siku 40 usiku na mchana,hadi safina ikatua katika mlima Ararati(Uturuki ya sasa),akaokoa wanyama wawili wawili,ndege,wadudu,mijusi n.k na anasema hataua tena watu,kwamba alileta upindi wa mvua kama ishara ya suluhu,hataua waovu tena!
Huu ni msimamo wa Wamarekani hawa sasa wanaopinga Biblia na unabii wake.
 Wanyama walioingia safinani zama za Nuhu walikuwa  takriban 45,000 wakati binadamu waliosikia sauti ya Nuhu walikuwa jumla wanane wa familia moja tu,miongoni mwa wakazi hao wa dunia takriban bilioni 11 zama hizo walioangamizwa na gharika.
Leo,dunia ina watu bilioni 7.1.
“Zaidi ya watu bilioni 11 walikataa wokovu zama za Nuhu,wakaangamizwa kwa gharika,wakati watu wanane wakikubali”,na jambo hilo linazamwa kama hadithi za kutunga,za Mungu kuangamiza mabilioni ya watu kwa kutumia majanga kama Katrina huko Amerika.
Sasa,Bobby Jindal na Rick Perry,wanasema majanga ya asili kama Katrina  naJoplin huko Missouri, yaliyoua maelfu ya watu,yameletwa na Mungu huyu wa akina Carson, sasa kwamba “Mungu huyo mkatili ndiye amewapa haki Wakristo kama Carson kuitawala Marekani?”
Wanajiuliza Wamarekani.

Wamarekani wamekataa kuiamini Biblia hii, wanasema inawasaidia kuishi tu kwa kutumia mashauri yake,kwani wengi wamelelewa kuwaamini akina ‘Father Christmas’ ,Santa Claus, na wanamwona Yesu kama wa kufikirika tu,hawaoni sababu kuendelea kuamini na kusumbua nafsi zao kwa imani hizo!
 Za kufikirika!
Hata hivyo,Biblia katika Ufunuo wa Yohana 13:11 inasema Marekani(Mnyama mfano wa mwanakondoo aliyeinuka bila vita huko Bara la Amerika),angebadilika na kusema kama asemavyo Shetani.
Wanazuoni wa Biblia wanasema hawashangazwi na Wamarekani kusema Mungu hayupo,kisha kuwa na mashaka na Biblia kwamba ilitabiriwa miaka 1680 kabla ya Marekani kupata uhuru,kwamba Wamarekani na serikali yao wangetilia shaka kuwepo kwa Mungu na uhalali wa Biblia Takatifu.
Mamilioni ya Wamarekani ni Wakristo wa Ki-Protestanti waliokimbia vita Ulaya katika karne ya 16.
 Huyu,Ben Carson Jumatatu iliyopita alitoa kauli nyingine iliyowachefua wa-Misri,kwamba ma-Piramidi yaliyojengwa miaka takriban 4,500 iliyopita,yalijengwa na Yusufu kama maghala ya kuhifadhia nafaka.
Wa-Misri wanaamini mapiramidi yalijengwa kama makaburi ya ma-Pharaoh

Majengo haya yaliyodumu kwa millennia nne-unusu,sasa yanasimuliwa katika harakati za kuwania uteuzi wa Republican Marekani,hadi kusababisha hata Misri kumdharau Carson kwamba ameacha Udaktari wa upasuaji wa mishipa ya fahamu na ubongo,sasa anarukia Urais wa Marekani huku akisema-sema maneno ya kukariri Biblia(kitabu cha Mwanzo).
Majuma mawili yaliyopita,Carson alisimamia imani yake kwamba, “Mapiramidi ya Misri yalijengwa na Mtu Mkuu wa Biblia,Yusufu ili kuhifadhi nafaka zama zile za miaka ya njaa,badala ya kukubaliana na wanasayansi kwamba yalikuwa makaburi ya ma-Pharaoh.
Associated Press limesema Mkuu wa sekta ya Mambo ya Kale katika wizara ya Mambo ya kale,Mahmoud Afif,alijibu kusema kauli ya Ben Carson haina ithibati yoyote(siyo sahihi), ni dhana tu kuhusu mapiramidi,ni kauli zinazofanana na wanaosema yalijengwa na watu toka bara lililopotea.
Kuna video imewekwa kwenye mitandao Jumatano iliyopita na Buzzfeed News ikisema Carson alitoa  dhana hiyo miaka 17 iliyopita huko Chuo cha Michigan kinachoongozwa na wa-Adventista wa Sabato.
Katika video hii,Carson anasema, “Kwa mawazo yangu binafsi ni kwamba Yusufu alijenga Mapiramidi ili kuhifadhi nafaka”.
Alikuwa akizungumza kuhusu Agano la Kale linavyozungumza habari za Yusufu akitabiri miaka saba ya njaa katika Ikulu ya Pharaoh wa Misri,akimshauri kuweka akiba ya chakula(Mwanzo  sura 39-45).
Hii ndiyo kauli ya Ben Carson kwamba mapiramidi yalijengwa na Yusufu(Joseph)kwa nia ya kuhifadhi nafaka.
Akasisitiza, “Naamini biblia kama watu wengine wafanyavyo,na sioni kama ni ujinga kufanya hivyo ingawa maendeleo ya kisekula yanazidi kutucheka tunaoiamini,na tuko radhi kukaribisha dharau hizo”,  Benjamin Carson alisema.

"MWADVENTISTA NA SIASA"JE NI SAWA KUWA MWANASIASA HUKU IKIWA MWADVENTISTA?


NI KIPINDI MAALUM CHA MJADALA KILICHOHUDHURIWA NA WAUMINI WA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO TOKA NDANI NA NJE YA VIUNGA VYA JIJI LA MWANZA KATIKA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO KIRUMBA MWANZA TANZANIA.
BAADHI YA WATU MASHUHURI WALIOSHIRIKI MJADALA HUO NI MH. STEPHEN MAGOIGA, MFAMASIA NA MWINJILISTI PHILIPO JOSEPH, NDUGU MECK MANYAMA,MZEE SITTA NGISSA, NDUGU SAMUEL NKONYA, NDUGU JOSEPH NJILE,DR.ONDITI, DR. PRAYGOD NA WENGINE WENGI KWA USIMAMIZI WA MCHUNGAJI BEATUS MLOZI.
HATA HIVYO BAADA YA MAJADILIANO MAREFU TULIHITIMISHA KWA KUKUBALIANA YAFUATAYO:-
Sheria ya Mungu katika ulimwengu imejengwa katika utayari wa utii wa viumbe vyake alivyoviweka kwa ukarimu wake mkuu. Ni imani pekee ndiyo iliyosimikwa katika moyo wa mwanaadamu na kutegemeza kila tendo litakalosukumwa na upendo wake. Hakika hilo ndilo linalokubalika na Mungu. Upendo hata hivyo siyo msingi wa sheria za serikali. Kwa hiyo juhudi za kushinikiza imani kwa asili yake ni kinyume na dini ya kweli, na hili ni kinyume na mapenzi ya Mungu.
Kama Waadventista wa Sabato tunatambua mchango mkubwa unaofanywa na serikali zilizosimikwa katika jamii zetu. Tunapaswa kuziheshimu na kuziunga mkono kwa juhudi zote zinapokuwa katika harakati za kutekeleza majukumu yake. Ila pale tu itakapoonekana ya kuwa sheria ya nchi mahalia inapingana na mamlaka ya neno la Mungu, tunapaswa kusimama katika neno , maana ni bora kumtii Mungu kuliko mwanadamu. Waadventista wa Sabato tumeitwa kusimamia kanuni za uhuru wa dhamiri wakati wote tukiendelea kuwapenda na kuwathamini wengine.
Kanisa la Waadventista wa Sabato linatambua historia ndefu inayoonyesha namna watu wa Mungu walivyoshika madaraka na kushiriki katika shughuli za kiserikali. Yusufu alikuwa na madaraka ya kiserikali katika nchi ya Misri, vivyo hivyo Daniel, alipanda vileleni kimamlaka katika Babeli na matokeo yake taifa likafaidi kwa uwepo wao.
Kimsingi mivuto ya kisiasa si tatizo, Muadventista anaweza kujisikia kushikilia madaraka katika uongozi katika serikali, hata hivyo siku zote tunapaswa kuwa makini kwa hatari ambazo zinaambatana na mivuto ya kidini katika utendaji wa serikali na kudumu bila kuchoka kukwepa kwa makini hatari hizo.
Kila inapotokea Muadventista wa Sabato kuwa kiongozi, akitoa mvuto wake katika jamii anapaswa kufanya hivyo kwa kutumia kanuni ya dhahabu (Golden rule).
Tunapaswa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupiga kura unaopatikana katika maeneo yetu. Ikiwa inawezekana kufanya hivyo, basi tushiriki katika dhamiri safi na kuwajibika kikamilifu (GW 391, 392)
Waadventista wa Sabato hatupaswi kubobea katika masuala ya siasa na kuzitumia mimbari zetu au machapisho yetu kusukuma utawanyaji wa mawazo ya kisiasa.
Waadventista ambao ni viongozi serikalini wanapaswa kukubali na kuazimia kuweka maishani viwango vya juu vya maisha ya kikristo. Wawe akina Daniel wa kisasa na Bwana atawaongoza kutenda mapenzi yake na kuisaidia jamii kumjua Mungu.
Maonyo mazito yametolewa na Mama E. G. White dhidi ya masuala ya kisiasa na shughuli zake amesema, “Acha kabisa masuala ya siasa……. Kila mwalimu, Mchungaji au kiongozi katika ngazi za kanisa ambaye ana kusudia kupenyeza mawazo yake katika masuala ya siasa anapaswa kurejeshwa katika kuiamini kweli ama sivyo ajiuzulu katika wadhifa aliopewa” (GW 392, 393)
<IWAPO UMEBARIKIWA SEMA AMINA>

 

Copyright ©2015 KIRUMBA ADVENTIST CHURCH