SABATO YA TAREHE 23/5/2015 Wasabato watakiwa kurejea tabia ya Kanisa la Mitume


"Nawaambia hivi, Kuomba kwa nia ya kufanya matengenezo ni lazima....",Mchungaji Beatus Mlozi
Yasisitizwa, bila kufanana na Mitume,hakuna atakayemwona Mungu!
Na Conges Mramba,Mwanza
MKURUGENZI wa Idara ya Uchapaji katika Jimbo la Kusini mwa Ziwa Nyanza(SNC),Beatus Mlozi,amesema Washiriki wa Kanisa la Waadventista wa Sabato wanapaswa kufanya Matengenezo na kurejea tabia zilizokuwemo katika Kanisa la Mitume.
Mchungaji Mlozi amesema Kanisa la Mitume liliongezeka idadi ya washiriki wake na viwango vya Ubora wa kiroho,kwa njia ya Kujifunza pamoja Neno la Mungu,Kushiriki Meza ya Bwana,kupendana wao kwa wao na kudumu katika maombi.
Akihutubu Huduma Kuu katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Kirumba,Jijini Mwanza Sabato mchana,Mei 23,Mchungaji Mlozi amemtaka kila mshiriki wa Kanisa kufanya Matengenezo, ili kufanana na Kanisa la Kwanza la Mitume.
“Ni jambo muhimu kwa kuwa hakuna atakayeingia Mbinguni asipokuwa na Utakatifu uliokuwemo miongoni wa washiriki wa Kanisa la kwanza la Mitume.”,amesema Mch.Mlozi.
Kauli ya Mkurugenzi huyo wa Idara ya Uchapaji ya South Nyanza Conference, imekuja kukiwa na changamoto ya washiriki wapya kutodumu katika Ushirika,kufuatia hali ya washiriki wa zamani kupooza na kutokuwa na viwango vya Ubora kama vinavyoainishwa katika tabia za Kanisa hilo la Mitume.
“Kama kanisa linakua,nawe mshiriki hukui, maana yake hauko kwenye kanisa lile.”amesisitiza.
Kanisa la Mitume lilikua kwa njia ya waumini wake kuongezeka kufuatia kusikia Injili.
“Kanisa linakua kwa njia ya Kuhubiri Injili,kanisa linalokua ni lile linalohubiri Habari Njema ya Wokovu”,amefafanua.
Alisema, washiriki wa Kanisa la Mitume walidumu kanisani wakimega mkate;wakishiriki chakula chao kwa furaha, wakiwapendeza watu wote.
Akaonya kwamba leo Washiriki wameshindwa kula chakula pamoja,na kwa sababu kanisa limepoteza ushirikiano, Kanisa limepoteza hata tabia zilizokuwemo miongoni mwa washiriki wa Kanisa la zama za Mitume(1-100 `AD).
Alifafanua kuwa Kanisa la Mitume walizingatia vitu vitano:
• Walidumu katika Chumba cha Juu(Upper Chamber) wakiomba na kungoja ahadi ya Roho Mtakatifu.Wenye chuki na magomvi miongoni mwao hawakudumu katika chumba hicho cha Juu. Walitunza mahusiano ndani ya Kanisa
• Waliodumu chumba cha Juu wakingoja Roho Mtakatifu,walisameheana,wakatengeneza Umoja(Matengenezo)halisi ya kiroho-Spiritual Reformation, ni muhimu katika Ujenzi wa Kanisa leo.
Walidumu kusubiri Roho Mtakatifu,Walidumu katika Mafundisho ya Mitume,ni kujifunza neno la Mungu kwaa bidii nyingi.
• Walidumu katika Ushirika(Fellowship);ni udugu(Brotherhood);kutembeleana,kusaidiana na kubebeana mizigo.Kanisa la Mitume halikuruhusu familia moja miongoni mwao kulala njaa.
• Kuumega Mkate(Lord’s Supper) na Chakula cha kawaida wanachosaidiana washiriki wanapokula pamoja.Familia zilikuwa na tabia ya kula pamoja chakula,kwa sababu hiyo, upendo wa kidugu(Brotherhood)ulidumu miongoni mwao.
• Maombi huongeza ubora wa ubora wa kiroho,na kumfanya Mshiriki wa Kanisa kuzungumza na Mungu;ni kukiendea Kiti cha Rehema.
“Hiyo tabia ya kula chakula pamoja imekwenda wapi? Hata tabia ya kula makande pamoja imekwenda wapi?”Pr.Mlozi akahoji.
Kufuatia hali hiyo, washiriki walishikamana. “Mshiriki anayekuja kukutembelea,amechukua sehemu ya maisha yake kukuthamini”,amesema.
Akasisitiza kwamba washiriki wametakiwa kurejea tabia ya Kanisa la Mitume kwa kutenda haya na kuutafuta Utakatifu ambao hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao.

Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

 

Copyright ©2015 KIRUMBA ADVENTIST CHURCH