Kwanini waovu wanapendwa na kulindwa sana na Mungu kuliko Wema?


Kwanini waovu wanapendwa na kulindwa sana na Mungu kuliko Wema?
• Vyombo vya ghadhabu vinaruhusiwa kutekeleza agenda zake!
Na Mwandishi Maalum,Kirumba
MKURUGENZI wa Vijana,Muziki na Chaplensia katika Union ya Kaskazini mwa Tanzania(NTUC),Pr.Elias Kasika, amewataka wa-Adventista wa Sabato kushukuru na kustahimili mema na mabaya yanayowatokea,kwa kuwa Mungu anaruhusu kila jambo litokee kwa makusudi ya wokovu.
Akizungumza katika Ibada maalum ya shukrani kwa Mungu katika kanisa la wa-Adventista wa Sabato Kirumba Jijini hapa, Novemba 28 amesema kwamba haiwapasi wanadamu kumlaumu Mungu kwa kuwa waovu wakiwemo mafisadi wanalindwa na Mungu kuliko watu wenye haki.
“Wabaya wanalindwa na Mungu hata watakapomaliza kufanya kazi yao ya ubaya,maana waongo na wadanganyifu kama Yakobo walipendwa sana na Mungu kuliko hata waaminifu kama Esau”,alisisitiza Pr.Kasika huku akikariri Biblia takatifu katika kitabu cha Mwanzo,Warumi na. Zaburi.
Akawashauri wenzi wa ndoa kumshukuru Mungu hata ndoa zao zinapoingia katika machafuko,ili agenda ya Mungu ipate kutekelezwa.
Hapa,Pr.Kasika alikuwa akikemea tabia ya watu kutengana ama kuachana na wenzi wao wa ndoa kwa kisingizio cha ukatili,ubaya na hiana miongoni mwao.
Akasema pia kwamba hata wanasiasa wanakasirika na kuiingiza nchi yetu katika vurugu kwa kushindwa kutambua kwamba Mungu ndiye atawalaye katika dunia,na agenda zake zinapaswa kutekelezwa wakati wa Pambano kuu baina ya ubaya na wema.
“Kaini alikuwa chombo cha ghadhabu,alipewa fursa kutenda mema akachagua kumuua nduguye Abeli aliyekuwa mwema,lakini bado Mungu alimwekea ulinzi ili asiuawe.Watoto wa Kaini Mungu aliwalinda na kuwapa ujuzi na vipawa vya muziki wa hali ya juu na uwezo wa uhunzi”,Pr.Kasika alisisitiza.
Amehoji kama wataalam wa teknolojia ya hali ya juu wote ni waaminifu,lakini akasema Mungu huwabariki hata waovu wanaofanya maajabu katika dunia leo, hata hivyo waaminifu wa Mungu wanapaswa kushukuru kila jambo.
“Kama watu waaminifu hawataki kushukuru kila jambo,basi huenda wanaweza kuliacha kanisa wa wakaamua kuasi”,amesema,huku akieleza mateso aliyopata Paulo wakati alikuwa mtumishi mwaminifu wa Mungu.
Amesema pia kwamba,wala si ajabu kwa watu waaminifu wa Mungu kupata ajari,kufa au kuvunjika miguu wakiwa katika kazi ya Mungu,kwa kuwa vyombo vya ghadhabu(uovu)vimeruhusiwa kuendelea kufanya kazi duniani.
Akahoji, ‘Ni wangapi watakaomshukuru Mungu katika mabaya yaliyotokea? Je,kama wewe ni mume au mke,utakwendaje kumshukuru Mungu kwa sadaka za shukrani kama hujamsamehe kwa mabaya aliyokutendea?”
“Pendo la Mungu linakuongoza kwa kukuumiza ili ufikirie kuungama,siyo kulaumu na kushindwa kumsamehe mwenzako aliyekuumiza!” Pr. Kasika alisisitiza.
Baadhi ya wageni waliohudhuria katika ibada ya jana Kirumba ni pamoja na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza,Miraj Mtaturu, Mbunge wa Ilemela(CCM)Angelina Mabula,Mwenyekiti wa Jimbo la SNC la wa-Adventista wa Sabato,Pr.Zadock Butoke,Mkurugenzi wa Afya wa NTUC,Dk.Silas Kabhele,Mkrugenzi wa Mawasilano wa SNC,Pr.Beatus Mlozi ,viongozi wastaafu wa serikali na madiwani mbalimbali katika jiji la Mwanza.
Akitoa shukrani,Katibu wa CCM mkoani Mwanza,Miraj Mtaturu amesema Kanisa la wa-Adventista wa Sabato ni sehemu ya Jamii ya wa-Tanzania wanaopaswa kuthamini umoja.
Amesema kuwa kiongozi wa umma ni kuwa mtumishi wa Mungu katika sekta za umma,akaomba kanisa kuwaombea kwa Mungu,kwa kuwa unapogusa maslahi ya watu wabaya ambao ni wachache kulinganisha na wengi wabaya.
‪#‎SHARE‬ NA WATAKATIFU WENGINE WA BWANA

Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

 

Copyright ©2015 KIRUMBA ADVENTIST CHURCH