SABATO YA TAREHE 6/6/2015. Muziki wa Kikristo, kichocheo cha afya na tiba.

Na Conges Mramba,Kirumba


SEMINA ya Muziki iliyoanza  Jumatano,Juni 3 imetia nanga Katika Kanisa
la  Waadventista wa Sabato Kirumba Jijini Mwanza  Sabato ya Juni
6,huku Jamii nzima ya waimbaji nchini Tanzania ikitakiwa kumtukuza
Mungu kwa kuimba nyimbo zenye kuzingatia Kanuni, Biblia na Roho ya
Unabii.
Mkufunzi wa semina hiyo,Dk.Samweli Tumaini Mugaya(PhD), ambaye ni
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma, amesema aghalabu nyimbo huimbwa nje
ya taaluma na kanuni mahsusi za uimbaji,
Akitoa mfano,amesema waimbaji huimba pasipokufuata mapigo ya
nyimbo,hali inayosababishwa nyimbo kuimbwa vibaya hata pasipo
kuzingatia tune husika za nyimbo nyakati za ibada.
Dk.Samweli Mgaya amesisitiza uimbaji bora unaozingatia maadili ya
taaluma ya muziki ili kufariji washiriki na kuinua myoyo yao kwa
Kristo nyakati za Ibada.
“SAUTI NYINGI,WIMBO MMOJA”ndiyo kauli mbiu iliyotumika wakati wa
mafunzo hayo ya taaluma ya kuziki katika Kanisa la Waadventista wa
Sabato,ambayo yaliwahusisha washiriki wa makanisa ya Jijini Mwanza.
Hata hivyo,Dk. Mugaya amesema uimbaji una faida mbalimbali kiafya,kwa
kuwa huondoa msongo wa mawazo(Stress),huimarisha kinga ya
mwili,huwafanya waimbaji kukumbuka mafundisho ya kiroho,wakati pia
nyimbo hufariji na ni maombi halisi kwa Mungu.
Kulingana na TAFSIRI ya Shirika la Afya la Umoja wa
Mataifa(WHO)iliyotolewa mwaka 1948,Afya ni Ukamilifu wa
Kimwili,Kiroho,Kiakili na Mahusiano ya kufaa na Jamii nzima.
“Kwa sababu zilizotajwa na WHO,uimbaji huwafanya waimbaji kuwa na
mahusiano mazuri,kwa kuwa hukaa muda mrefu wakiimba pamoja na
kudumisha udugu na upendo”,Dk.Mugaya amesisistiza.
Akawashauri waimbaji kuzingatia mazoezi ya mwili na kanuni ya chakula
bora,unywaji wa maji salama  ya kutosha,huku wakiepuka vyakula vya
chumvi nyingi  na soda.
“Mboga za majani,matunda na viungo kama vitunguu saumu ni muhimu kwa
watu wanaojikuta sauti zikikwama”,amesema.
Akichangia,Mwalimu wa Kwaya ya Kirumba,Dk.Darlington Onditi,amesema
jamii ya vinywaji aina ya soda kwa waimbaji,huwasababishia sauti
kukwama.
Waimbaji pia wameshauriwa kutokukaa kwenye viyoyozi muda mrefu,kwa
kuwa  mapangaboi na viyoyozi huwa na tabia ya kukausha sauti pindi
wanapoimba.
“Tujitahidi kutumia hewa safi ambayo Mungu ameiumba,badala ya kutumia
hewa zisizoasili;ambazo huathiri afya hususan kwa waimbaji”,Dk.Mugaya
amesisitiza.

Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

 

Copyright ©2015 KIRUMBA ADVENTIST CHURCH