HUDUMA YA UTANDAAJI KATIKA KITUO CHA WATOTO WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU YAFANA.

Na Kamati ya Mawasiliano Kirumba.
Mnamo tarehe 30/05/2015 Jumamosi siku ya Sabato, Watoto wa kanisa la Waadventista Wasabato Kirumba walifanya huduma ya utandaaji katika kituo cha watoto waishio katika mazingira magumu wanaolelewa na kituo cha Foundation Karibu Tanzania. 
Watoto walishirikiana kuimba pamoja, mafundisho ya neno la Mungu yalitolewa. na Mkuu wa Idara ya Watoto kanisa la Kirumba mama Debora Ngissa akishirikiana na walimu wa watoto wa kanisa hilo Bi Betty Njile na Bi Eza Kabuche walikuwa wawezeshaji wa tukio hilo makini.
Aidha kanisa la Waadventista Wasabato Kirumba kupitia idara ya watoto ilitoa zawadi ya dawa ya kutibu vidonda na pesa tasilimu ya kununulia chakula kwaajili ya watoto wa kituo hicho. Kwa ujumla watoto na walezi wa kituo hicho cha Foundation Karibu Tanzania wamefarijika sana na kutoa shukrani zao za dhati kwa kanisa la Kirumba kupitia Idara ya watoto kwa jinsi inavyojali na kuonesha kwa vitendo Upendo wa Mwenyezi Mungu.

   MATUKIO ZAIDI KATIKA PICHA









Tupe maoni yako hapo chini..!

Share this article :

'LIKE' UKURASA WETU WA FACEBOOK HAPO CHINI...!

0 comments:

Post a Comment

 

Copyright ©2015 KIRUMBA ADVENTIST CHURCH